Entrepreneurship Skills

Entrepreneurship Skills Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Entrepreneurship Skills, singida town, Singida.

SAMSUNG GALLAXY S2 MPYAA IKO SOKONI-150000
26/03/2016

SAMSUNG GALLAXY S2 MPYAA IKO SOKONI-150000

19/02/2016

UONGOZI NA USIMAMIZI WA BIASHARA NDOGO NDOGO

Mjasiriamali anawajibu muhimu sana katika menejimenti ya biashara. Menejimenti
maana yake ni kuendesha biashara kwa ukamilifu. Katika kuendesha biashara
mjasiriamali anatekeleza majukumu / kazi mbalimbali:

a) Kuweka mipango:

Mjasiriamali anakuwa na mtazamo wa mbali na kuweka mawazo yako katika mpangilio
mzuri kwa namna ambayo anataka kutekeleza jambo lolote hapo baadaye. Kuweka
mipango kunamsaidia mjasiriamali kutekeleza kikamilifu kazi na program zake.

b) Kusimamia:

Mjasiriamamli anahakikisha kuwa kulingana na uwezo wao kuna mgawanyo mzuri wa
kazi kwa wafanyakazi na kuwapa mamlaka baadhi ya wafanyakazi katika baadhi ya
majukumu ya kibiashara.

c) Kudhibiti:

Mjasiriamali anahakikisha kuwa biashara inaendelea na kufikia malengo yaliyowekwa,
anafuatilia kwa makini na kuona kazi zinafanyika ipasavyo.

d) Kuratibu:

Mjasiriamamli anajukumu la kuratibu shughuli mbalimbali katika biashara. Ratiba ya
kazi lazima ifuate mpango wa kazi kwa kuratibu rasilimali watu na mahitaji ya uzalishaji
(mafano. malighafi).

e) Kuelekeza:

Mjasiriamali anatakiwa kuona kuwa kazi zinazotakiwa kufanyika zinatekelezwa.
Majukumu ya meneja ni kuhakikisha kuwa shuguli zinakamilishwa kwa ama kupitia
yeye mwenyewe au kupitia watu wengine.

f) Kuwapa motisha:

Endapo mjasiriamali ana wafanyakazi, anatakiwa kuwa na mahusiano mazuri na watu
wake, kwani wafanyakazi wanaweza kumfanya afanikiwe au kushidnwa. Wafanyakazi
wanahitaji motisha na mazingira mazuri ya kazi.

04/02/2016

VIPENGELE VYA KUZINGATIA KATIKA KUCHAGUA WAZO LA BIASHARA (Business idea)

1.Aina ya bidhaa/huduma
2.Ubora na bei ya bidhaa zako vikoje ukilinganisha na bidhaa za washindani wako?
3.Biashara itafanyika wapi?
4.Nimaeneo gani biashara yako itapata wateja?
5.Wateja wa biashara yako ni akina nani?
6.Inawezekana kukadiria bei ya bidhaa hiyo kwa sasa?
7.Bishara yako inaweza kuk**ata sehem gani au asilimia ngapi ya soko?
8.Bidhaa yako itauzwa kwa bei ipi?
9.Nikiasi gani cha bidhaa zitauzwa?
10.Je ni mbinu gani za matangazo zitatumika kuuza bidhaa zako
11.Nimbinu gani zinahitajika kuhakikisha kuwa makisio ya mauzo yanatimia?
12.Nivitu gani unahitaji ili kuvumisha na kusambaza bidhaa zako?

19/01/2016

VIGEZO AMBAVYO BANKI WAATANGALIA ILI KUKUPATIA MKOPO KWA AJILI YA BIASHARA (Criteria for assessing loan application)
Banki na taasisi nyingine za fedha nao pia ni wafanyabiashara na wanahitaji pia faida kwa kile wanachokifanya.Ili bank wakupe mkopo ni lazimaa wataangalia capacity na willingness uliyonayo katika ulipaji.Ili bank waweze kukupatia mkopo ni lazimaa waangalie vigezo (criteria)vipatavyo sita.
*CHARACTER (sifa)
-Bank itaangalia je una uzoefu katika biashara? (Experience)
-Bank itaangalia pia unaujuzi gan na biashara unayotaka au unayofanya(techn skills)
-Pi bank itaangalia k**a una sifa binafsi za mjasiriamali (apersonal entrepreneurial characteristics). eg. Risk taking,persistance,opportunity seeker, etc.

*CAPACITY-(uwezo)
Maofisa wa mikopo wataangalia mtiririko mzima wa fedha katka biashara yako na nikiasi gani pia cha faida unaweza kupata ndani ya mwezi mzima ili kuweza kuona nikisi gani unaweza kukopa pia wataangalia yor financial records nikiwa na maana kwamba Income, expenses and profit ili wawezo kufaham nikiasi gani unaweza kurejesha kwa wiki ama kwa mwezi..
Pia wataangali mpango wako wa bishara (business plan) katika business plan wataangalia Aina ya product,market plan ,production plan, management etc.

*CAPITAL-(mtaji)
Banki nyingi unapoenda kukopa watahitaji walau uwe na asilimia 30 ya mkopo ambao unataka kuchukua..Kwamfano Endapo unataka mkopo wa SH 500000 ya kununulia mashine ya kuchomelea banki itakuhitaji walau uwe na asilimia 50 ya ule mkopo unaouhitaji kwa maana hiyo utapaswa uwe na mtaji wa thamani ya sh 25000..

*CREDITY HISTORY
-Hapa sasa banki wataangalia k**a je ulishawahi kukopa hela hapo kabla?
-Na je k**a ulishawahi kukopa huwa unalipa kwa wakati?
-Pia banki wataangalia k**a ulishawahi kukopa na ukamiss kulipa?
Tutaendelea na kigezo cha 5 na 6

15/01/2016

Types of financial institution in Tanzania
~There are many financial institution in Tanzania that offer finanancial services for small business..these include
*Banks like NMB,CRDB,AKIBA COMMERCIAL BANK,BANK OF AFRICA
*Micro financing institution like PRIDE,FINCA,SEDA
*Saving and credit cooperative societies (SACCOS)
*Informal saving and credit groups like VIVOBA, Rotating savings and credit associations (ROSCA)

04/01/2016

TABIA MBAYA KUMI ZINAZOFANYA USHINDWE KUWA NA AKIBA "SAVINGS"....HATIMAE UNAKOSA MTAJI WA KUFANYA MAMBO YAKO...
1.Unanunua nguo bila mpangilio..
Kuna watu wana nguo k**a duka. Plz Kuwa na nguo chache Tu huwezi kushindana na fashion.
2.Unanunua Viatu bila mpango.
Viatu pia vinameza savings zetu. Nunua pea chache zenye ubora ili zidumu.
3.Unatoa ofa bar bila mpango.
Nenda bar kwa bajeti mahususi. Hakuna atakae kusifia kwa kutoa ofa hovyo. Kila mbuzi ale kwa urefu Wa kamba yake. Jifunze ubepari.
4.Unatumia hela nyingi kwenye simu ambazo sio productive. Unaweka vifurushi vya week vya sh 7000 au 10000 ili uchati na marafiki Fb au wasaap Huo ni ujinga. Badilika.
5.Unakopa hela benki na kununua vitu k**a simu ya milioni na gari ambazo sio productive. Unakosa hela hata ya mafuta, gari la nini kwanini usingewekeza sehemu ili kuwe na mradi Wa kuzalisha ndio ununue gari?
6.Una marafiki wengi ambao ni mizigo kwako au hamuendani kivipato hivyo unajikuta unalazimika kutumia zaidi ya kipato chako ili uwa-impress. Meneja Wa TRA na mwalimu Wa sec unatarajia utoe offer mpaka umfurahishe meneja? Utabaki na sh ngapi toka kwenye salary yako?? Zinduka.
7.Huna timetable ya kudumu ya maisha yako, unajikuta unaburuzwa Tu na marafiki zako kwa kwenda sehemu mbalimbali za matumizi.
Kuwa na ratiba za maisha yako na zisimamie kikamilifu, usiburuzwe!
8.Una michepuko inayokutegemea wewe kwa kila kitu. Wanakuita ATM we we unakenua Tu huzinduki. Badilika.
9.Una huruma sana kuliko kipato chako. Yaani kila ukiombwa unatoa hata k**a muombaji hana genuine need. Usiwe mkristo kuliko Yesu. Fanya hivyo k**a ni lazima. Ila sio kila anaekupiga mzinga unapigika.
10.Unatembea na hela nyingi kwenye wallet au mshahara wote kwenye wallet au handbag au nyumbani kwako. Unapokuwa na petty cash nyingi unatengeneza mazingira ya kutumia hovyo. Jifunze kuweka hela benki. Tembea na hela Tu unayoihitaji kwa matumizi ya lazima.
Naamini tukizingatia kanuni hizi kumi tutaongeza savings zetu na kuwa na mtaji Wa kufanya vitu vikubwa endelevu
Mjasiriamali ni mwenye kuona fursa zilzopo katka eneo linalomzunguka na kuweza kuztumia vyema na katka ubora na kiubunifu zaidi..thnk differentl y

02/01/2016

Source of finance for small business
~Own assets
~loan from family and friends
~loan from financial institutions. Eg Banks
~Retained profit from the business
~personal savings

21/12/2015

JINSI YA KUWASHAWISHI WATEJA KWA NJIA YA BEI

Bei sahihi/inayokubalika ya bidhaa/huduma ni muhimu ili kufanikiwa katika biashara.
Ikiwa bei ni ya chini sana uwezekano wa kupata faida ni mdogo, na k**a bei ni ya juu
sana wateja hawatakuwa tayari kununua.

Kuna njia tofati za kumvuta mteja kwa bei:

a. Bei ya kuuzia (SELLING PRICE)

Watu wataangalia bei unayouzia na kulinaganisha na ubora wa bidhaa unayouza, na
bei za washindani wako n.k. Kiwango cha bei unayouzia kinatokana na sababu
mbalimbali; ghrama ya kuzalisha, kiwango cha faida; soko na ushindani katika soko.
Sehemu hii itaelezewa kwa kirefu zaidi katika kipidi cha ghrama za uzalishaji na bei ya
kuuzia 'Costing' and 'Pricing'.

b. Punguzo la bei (DISCOUNTS)

Wateja wanaweza kuvutiwa panpokuwepo na puguzo la bei k.m:
- Punguzo la bei kwa kunua kwa fedha taslimu: wateja wanaolipa fedha taslimu
hupunguziwa bei kuliko wanaonunua kwa mkopo.
- Punguzo la bei kwa wanunuzi wa jumla/wanaonunua vitu vingi kwa wakati
mmoja: Wateja wanaonunua kw wingi kwa wakati mmoja hulipia bei ndogo kwa
kila bidhaa.

c. Zawadi maalumu itolewayo kwa kununua bidhaa (SPECIAL OFFER)

Wateja huvutiwa na zawadi zinazoanbatana na kununua bidhaa k.m:
- Unaponunua paketi ya sigara hupewa kiberiti bure.
- Unaponunua viatu unapewa kamba za ziada za kufungia bure.

d. Upendeleo maalumu wa kulipia (FAVOURABLE PAYMENT CONDITION)

Wateja wanaweza kuvutiwa kunua iwapo wanapewa upendeleo wa kulipa kidogo
kidogo. Hata hivyo ni budi kuwa mwangalifu kwa kuuza kwa mkopo. Fanya hivyo kwa
wateja wachache na wenye kuaminika! (Angalia pia kipindi cha usimamizi wa fedha).

Hitimisho:
Vigezo vingi vinahitajika kuangaliwa katika kupanga bei:
- Ghrama za uzalishaji
- Kiwango cha faida
- Bei za washindani wako
- Kiwango cha bei ambacho kinakubalika na wateja wako
Bei pia inaweza kutumika katika kuwavutia wateja na hivyo kuitangaza bidhaa yako

10/12/2015

KUTAMBUA NA KUTATHMINI FURSA ZA BIASHARA.

Nini maana ya Fursa bora?

Mjasiriamali ni mtafutaji fursa. Kazi yake ya kwanza ni kutambua na kuchagua fursa
inayovutia au yenye manufaa. Nini maana ya fursa? Kwa lugha rahisi inaweza ikawa
na maana ya uwezekano wa mradi kufanikiwa.
Utambuzi wa fursa za biashara unahitaji juhudi za ziada na ujuzi maalum. Hta hivyo
kwa wakati wowowte panahitajika vigezo na miongozo itakayosaidia kutambua na
kutathmini fuursa vipo kwenye ngazi ya maeneo husika .Vigezo hivyo ni pamoja na:

A: MAZINGIRA

- Hali halisi ya eneo na rasilimali zilizopo zake.
- Watu, aina za kazi/ajira iliyopo na jamii na hali yao kiuchumi

B: MWONEKANO WA BIASHARA ZILIZOPO.

- Hali halisi ya shughuli za biashara zilizopo katika eneo husika kwa
kuhusiamisha na mwingiliano wa bidhaa kutoka katika maeneo jirani,
uwezo wa soko, mahitaji ya bidhaa na huduma za viwandani.
- Mwelekeo na muundo wa shughuli za kibiashara kwa kuzingatia mahitaji
mapya ya bidhaa na huduma kwa wateja katika eneo husika.

C: WALENGWA (WATEJA).

- Matarajio, uwezo na mapungufu yao.(k.m. vile ujuzi, maarifa/ufahamu, hali
ya kifedha n.k.
YAFUATAYO YANAWEZA KUWA MBADALA WA KUSAIDIA KATIKA KUTABUA FURSA YENYE UWEZEKANO WA KUTEKELEZEKA KATIKA ENEO LOLOTE LILE.

(1) RASILIMALI

Viwanda vinavyojihusisha na madini, kilimo, uvuvi na maliasili nyinginezo..
Bidhaa zinazotokana na masalia/mabaki ya kilimo, miti/mbao na metali.

(2) MUUNGANIKO

Viwanda vinavyotokana na muunganiko mbalimbali k**a vile viwanda
ambavyo malighafi yake yanatokana na masalia ya viwanda vingine au
kiwanda kimoja kutegemea kiwanda kingine kwa malighafi katika
uzalishaji na kinyume chake.
- Miradi inayosaidia maendeleo
- Viwanda vinavyojihusika na uandaaji wa bidhaa zinazosafirishwa
nje au uunganishaji wa bidhaa zinazotoka nje ya nchi au nje ya
eneo husika.

(3) BITHAA ZIZOSAFIRISWA NJE/BITHAA ZISIZOKAMILIKA ZINAZOINGIZWA KUTOKA NJE.

Kwenye maeneo mengine kuna uwezekano wa baadhi ya bidhaa aidha
kuingia kutoka nje ya nchi au kusafirishwa kwenda nje ya nchi.Bidhaa
za aina hiyo zinatoa fursa nzuri katika kuendeleza tasnia
zinazojihusisha na usafirishaji na uingizaji wa bidhaa nje na ndani ya
nchi. kati ya hivi vitu viwili,uingizaji wa bidhaa kutoka nje zisizo kamilika
unatoa fursa nzuri inayovutia katika biashara. Katika hali hii siyo tu
uwepo wa bidhaa ndicho kinachovutia bali pia soko lilishakuwepo.
(4) KUBADILIKA AU KUKUA KWA SOKO.

Baadhi ya wateja(walaji) na bidhaa za viwandani zinaasili ya kukua
kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu na uwezo wao wa
kununua, mabadiliko ya mtindo wa maisha au kiwango cha maisha.

(5) BITHAA MUHIMU/MAALUM

- Bidhaa zinatokana na utafiti na ubunifu.
- Bidhaa zitokanazo na ujuzi/maarifa
- Bidhaa zitokanazo na manunuzi ya taasisi/serikali au hosipitali/shule
- Bidhaa zitokanazo na ushirikiano na mataifa/viwanda vya nje

(6) SEKTA YA HUDUMA

- Uanzishwaji wa kitengo cha huduma ya matengenezo na ukarabati
wa nyumba husaidia katika kutoa huduma hiyo viwandani na
majumbani pia

09/11/2015

ZIFUATAZO NI SIFA AU TABIA BINAFSI ZA MJASIRIAMALI

(a) Kuthubutu

– Mjasiriamali huwa anatabia ya kuthubutu/kujaribu na
anafurahia changamoto, ila huwa hathubutu bila kuangalia faida na hasara
za kufanya hivyo. Kwa maana hiyo, yeye ni mtu anayethubutu au
anayejaribu kwa tahadhari.

(b) Kujiamini

– Kwa vile ana mawazo mazuri na uelewa mpana wa kutaka
kufikia malengo yake. Siku zote atakuwa anajiamini na anachokifanya.

(c) Ana mtazamo chanya

– Mjasiriamali anatabia ya kuona fursa za
biashara kwamba zinawezekana na hasa zile zilizoko kwenye mazingira
yake.

(d) Anapenda mafanikio

– Mjasiriamali siku zote anakiu ya mafanikio katika
ushindani wa kibiashara. Anafurahia kuzifanyia kazi changamoto
zinazomkabili na kuzikamilisha katika viwango vya hali ya juu. Pia anajua
uwezo na mapungufu aliyokuwa nayo katika kuendesha biashara.

(e) Anapenda kujitegemea

– Sifa hii ya kupenda kujitegemea ndiyo
inayomwezesha kuanzisha biashara yake mwenyewe. Mjasiriamali
anawajibika kwa kile anachokiamua na kukitenda. Anapenda sana kuwa
mkubwa (bosi).

(f) Anapenda kuwa na nguvu

– Mjasiriamali anapenda kushawishi wengine
na kuwaelekeza waweze kuyafanyia kazi mawazo yake.

(g) Mbunifu

– Mjasiriamali yuko tayari kuyapokea mawazo na maarifa mapya
kutoka kwa wengine na kuyatumia ipasavyo katika kuiboresha biashara
yake. Yuko tayari kuona kutoka kwa wengine mawazo mapya na
kuyatumia ipasavyo. Siyo kweli kwamba atachukua kila wazo. Atachukua
analoona linafaa na kuliachilia mbali wazo ambalo kwake siyo la msingi.
Mjasiriamali ni mtu anayependa kutafuta taarifa kutoka sehemu mbalimbali.

(h) Anaona mbali

– Mjasiriamali ana maono ya mbali na uwezo wa kutafuta
fursa za kibiashara kutoka kwenye mazingira ambamo watu wengine
wameshindwa kuona fursa hizo. Mjasiriamali ni mtu anayeona mbali siku
zote na muda wote anajiandaa kukabiliana na matatizo yatakayohatarisha
biashara yake.

(i) Ana uwezo wa kiuongozi

- Mjasiriamali ni kiongozi. Anauwezo wa
kuwafanya watu wapende na wawe na ari ya kufanyakazi kwenye biashara
yake. Wakati anaangalia biashara yake pia ana kasimu madaraka kwa
wafanyakazi wake ili awe na muda mwingi zaidi wa kufanya shughuli
nyingine k**a kuangalia ubora wa bidhaa, kutafuta masoko na masuala
mengine yanayohusu ubunifu.

(j) Mvumilivu na mchapakazi hodari

– Mjasiriamali anahakikisha kwamba
malengo aliyojiwekea yanakamilika kadiri ya uwezo wake. Mara nyingi yeye
mwenyewe ndiye mhusika mkuu wa kuhakikisha kazi inafanyika.
Anafanyakazi kwa bidii kuhakikisha malengo yanatimia. Hawezi/hapendi
kuona kazi haijakamilika.

(k) Ni muwajibikaji

- Mjasilimali anaamini kwamba yeye mwenyewe
anawajibika na matokeo ya maisha yake si mtu mwingine. Kwa
mjasiriamali, mafanikio ni tunda la juhudi zake binafsi, siyo bahati nasibu.
Anaongoza na kufanya mambo yaende wakati watu wengine wanafuata
nyayo zake. Anaanzisha wazo na kulifanyia kazi.

(l) Uwezo wa kushawishi na kuwafanya wengine wawe na ari

Mjasiriamali anauwezo wa kuzungumza na kuwavuta watu wengine. Watu
wote atakaokutana nao atahakikisha wanafanya anachofikiria yeye wafanye
kwa sababu wameshawishika na watafanya kwa hiari yao. Anauwezo wa
kuwavuta na kuwatia moyo.

08/11/2015

UJASIRIAMALI - Mchakato ambao mtu aidha akiwa peke yake au ndani ya taasisi
hutumia nafasi iliyopo kubuni vitu vipya au hufanya vitu ambavyo tayari vipo kwa njia
nyingine na kwa ubora zaidi.
Tafsiri ya ujasiriamali hutuwezesha kueleza vipengele vitatu vya msingi ambavyo
huainisha itikadi ya ujasiriamali.
ITIKADI YA UJASIRIAMALI huainishwa na:
a. Uhuru wa mawazo
b. msukumo wa kubadilika
c. vitendo
Yafuatayo hapo chini ni maelezo ya vipengele vya msingi vya itikadi ya ujasiriamali.

UHURU WA MAWAZO

Mojawapo ya kipengele kikubwa cha itikadi ya ujasiriamali ni uwezo wa kuwa na fikra
huru. Hii ina maana kuwa mtu yuko huru kufikiri bila kufungamanishwa na imani na
desturi zilizopo . Ni uwezo pia wa kutizama mazingira kwa akili iliyo wazi na tayari
kupokea mawazo mapya.Uhuru wa mawazo unahusishwa kwa karibu sana na fikra
bunifu na utafutaji fursa. Ni uwezo wa ‘kufikiri mbele ya kikomo’.
Ni k**a mjasiriamali mmoja aliyesema: “ Iwapo wote wanaelekea upande mmoja,
mimi natafuta upande wa tofauti yake”. Watu na taasisi ambao wana mawazo huru
hawabanwi na vizingiti vilivyowekwa na wengine. Siku zote hujiuliza: Kwa nini
wanafanya kwa namna ile na kwa nini nisifanye kwa namna ingine?

HAMASA YA MABADILIKO

Watu na Taasisi zenye itikadi ya ujasiriamali huainishwa na imani kuwa wao wana
uwezo wa kubadilisha 'Mazingira'. Wanaamini kuwa wanaweza kuamua waelekee
njia ipi. Kwa ujumla, hujisikia kuwa chanzo/kiini cha mabadiliko (internal locus of
control).
Imani kuwa (kazi, taasisi) 'hufanywa' , hufanya mtu na taasisi wasisubiri kuambiwa
cha kufanya na wengine. Chaguzi hufanyika kwa mtu kujihusisha pasipo kusubiri
kuambiwa. Huweka malengo yao wenyewe na kuweza kufanya uchaguzi ili kufikia
hayo malengo. Kwa sababu mtu anaamini uchaguzi wake ni sahihi, atawajibika
kufikia lengo na ashughulike kwa ajili hiyo. Kwa mtizamo wetu, kigezo muhimu cha
kubadili tabia binafsi ni hamasa. Iwapo mtu ana hamasa ya kubadili itikadi yake basi
ataweza kuleta badiliko. Kuondoa vizuizi vya mabadiliko, watu wawezeshwe
kujifanyia tathmini ya tabia zao na itikadi zao:
- Wanajua nini kuhusu tabia zao wenyewe (self-knowledge) na wengine
wanajua nini kuhusu wao?
- Nini itikadi yao katika maisha/maisha kwao yana thamani gani?

MATENDO AU VITENDO

Kipengele cha tatu cha itikadi ya ujasiriamali ni kitendo chenyewe. Ingawaje yaweza
kuonekana kuwa bayana, katika ngazi hii,aghalabu mchakato wa ujasiriamali huishia
hapa . Bila kitendo thabiti hatuwezi kuzungumzia ujasiriamali. Ndiyo maana
huchukuliwa kwamba uwezo wa kufanya kitendo na kuleta badiliko linalokusudiwa ni
kipengele cha msingi cha itikadi ya ujasiriamali.

07/11/2015

What is Entrepreneurship?
Entrepreneurship is a process by which individual either on their own or in organisations pursue opportunities actively , which result in doing new thing or doing thing that are already being done in a new and better way

ENTREPRENEURSHIP ATTITUDE is characterized by
a)Freedom of thought
b)Motivation to change
c)Action

FREEDOM OF THOUGHT
-Foresight
-seeing opportunities
-creativity
-flexibility
-independence
-receptiveness
*This allow them to look at the environment with an open mind and get new ideas.

MOTIVATION TO CHANGE
-Self awareness
-positive towards changes

ACTION
-Risk taking
-drive to (achieve)
-power of persuasion
-initiative
*Without action we can not speak of entrepreneurship , that’s why we consider the ability to take action and implement the desired change as a basic element of an entrepreneurial attitude.

Address

Singida Town
Singida

Telephone

+255762277227

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Entrepreneurship Skills posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share